Imetosha! Nataka kuoa, nimefanya vitu vingi sana - Diamond Platnumz
Msanii wa muziki Bongo, Diamond Platnumz amefunguka kuhusu mipango yake ya kuoa na siku atakayoowa.
Diamond akihojiwa na Wasafi TV amesema ana kila sababu ya kuoa kwa sasa kwani ameshafanya mengi kwahiyo anahitaji kutulia kwasasa.
"Nimepanga nioe Valentine mwaka huu , valentine itakuwa siku ya Alhamisi, Ijumaa, Jumamosi mpaka Jumapili, so far iko hivyo ikitokea iko tofauti nitabadilisha, nataka kuoa mwaka huu nina kila sababu ya kuoa, imetosha nimefanya vitu vingi sana, yaani nimefanya vitu vingi yaani doh mambo mengi sana i need to settle down, nahitaji kuoa mwanamke atakayenisaidia kuhandle hivyo vitu ," amesema Diamond.
Comments
Post a Comment