PENZI TAMU[IV]

“Ungependa kula na mimi na tupige soga zaidi” Aliuliza Sosi kabla Suma hajakimbia.

“ah..wenzangu wataningoja” alijibu Suma

“Hapana, tunaweza kwenda kijijini na kununua cha hotelini, mie leo sili dona lao” alijibu Sospeter huku moyoni akiombea kwa miungu yake Suma akubali.

“We, tutawezaje kutoka kambini si ni kujitakia matatizo? Huoni geti kali?”Aliuliza kabla hajakubali baada ya ushawishi wa Sosi. Sospeter alimhakikishia kuwa hawatagundulika na wakakubaliana wakutane saa moja baadaye kwenye lango kuu la shule. Sospeter alianza kutafuta njia ya kuweza kutoka na kurudi jioni hiyo bila kujiletea matatizo yeye mwenyewe na Suma.

Baada ya kuhangaika kufikiri nini cha kufanya aliamua kwenda kwa mzee mmoja wa Kimang’ati aliyekuwa zamu kulinda lango la shule hiyo. Wala hakumchelewesha alimpatia shilingi mia tano na kumuomba chonde chonde amruhusu yeye na Suma waweza kwenda na kurudi kabla ya muda wa kulala ambao ilikuwa ni saa nne kamili za usiku. Mzee wa Kimang’ati kumbe hizo zilikuwa zake. Alizifinyanga hizo pesa kiupole na kuziweka mfukoni. Alimwambia akiwaona wanakuja basi atajifanya anazunguka upande wa pili na geti atalisogeza upande kidogo tu. Na kweli hivyo ndivyo ilivyokuwa kwani Sosi na Suma walipofika hapo majira ya moja za jioni wakati giza ndio limeanza kuingia kwa nguvu na kunyamazisha sauti za ndege yule mlinzi alizunguka upande wa pili wa kibanda na kujifanya hakuona kitu na pale tu walipotoka alifanya haraka kufunga geti kwa kufuli. Alikaa kuwasubiri warudi.

Kesho yake kama moto ulioanzishwa na cheche, uvumi mkubwa ulienea kati ya wachezaji kuwa Sospeter na Suma walienda kufanya ngono kijijini. Ulianza kama utani na mwisho chumvi zikaongezwa, limao, na pilipili. Na wengine wakanyunyiza na amdalasini. Mara habari zilipowafikia Suma na Sosi, hawakuchelewa kwenda kwenye ofisi ya Mkuu wa Kamati ya Mashindano. Walipofika walikuta walimu wao wa michezo wakiwa tayari wamewatangulia. Walimu walifurahi kuona vijana hao walivyomakini na walivyoamua kuweka mambo sawa kabla hajaaribika zaidi. Waliwaelewesha walimu kuwa hakukuwa na kitu kama hicho na walikwenda kwenye kale ka mgahawa kalioko gulioni. Walikiri kutoroka na kwa hilo ndilo kosa pekee ambalo walimu walikubali, na katika kuwapa adhabu waliwasimamisha kucheza mechi moja moja kwenye timu zao. Jambo hilo basi likazimwa kimya kimya na kiutuuzima. Hata hivyo, ule uvumi tu wa kuwa walikwenda kufanya ngono ulikuwa kama umewapa hamu na wakaamua kufanya kweli. Tatizo lilikuwa ni muda na mahali, maana kila kona kulikuwa na wanafunzi na shughuli.

Hawakupata nafasi ya kuweza kujificha mahali na kupeana mapenzi hadi siku ya mwisho ya michezo ambapo timu ya kina Suma ilichukua ubingwa na ile ya kina Sosi ikishika nafasi ya pili. Wakati michezo inafungwa rasmi ukumbi ulilipuka kwa furaha mara baada ya kutangazwa rasmi kuwa kati ya wanamichezo waliochaguliwa kuwakilisha mkoa wa Arusha kwenye mashindano ya Taifa Morogoro walikuwemo Sosi na Suma. Sospeter alitangazwa kuwa Kapteni wa timu ya mkoa. Kambi ya timu hiyo ilikuwa ni Arusha, kwenye shule ya sekondari ya wavulana wenye vipaji ya Ilboru.

Kabla hawajaondoka Karatu, walikuwa bado wanatafuta nafasi ya kupeana tunda walilokatazwa. Nafasi ilijileta karibu saa moja kabla ya kuondoka hapo. Wakati wanafunzi wanaagana, Suma na Sospeter walienda kwenye mojawapo ya vyumba vya madarasa ambapo kulikuwa hakuna mtu, tena mchana kweupe. Walienda mmoja mmoja bila mtu yeyote kuwashtukia. Kilikuwa chumba cha kidato cha tano C kilichotazama upande wa shamba la shule hiyo.

“Kuna mtu amekuona” Sospeter aliyekuwa ametangulia alimuuliza Suma aliyekuwa amevaa sweta zito la rangi ya damu ya mzee, suruali ya jeans iliyokuwa imechakaa magotini na viatu vya raba vya rangi nyeupe ambayo ilikuwa imechafuliwa na vumbi la Karatu na kuvifanya vionekane vya rangi ya udongo.

“Hamna, ulitaka kusema nini huku kwa kificho” Aliuliza Suma kwa aibu huku macho yake yakiangaza angaza kwenye madirisha. Hakukuwa na mtu na sauti za wanafunzi zilikuwa zinasikika kwa mbali wakiimba nyimbo mbalimbali za kufurahia kambi hiyo.

“Nilitaka nikubusu kabla hatujaondoka, maana tukiondoka hapa itakuwa ni michezo tu ili tupate ushindi kwa mkoa” Alisema Sosi huku akimvuta karibu Suma. Suma alijifanya hataki lakini alikuwa anataka. Moyo ulikuwa ukimuenda kasi, na tumbo kama limejaa vipepeo! Viganja vyake vililowa kwa jasho licha ya baridi la mji huo uliokuwa karibu na lile shamba maarufu la Shangri La ambalo linamilikiwa na kina Christian Jebsen na Dr. Klatt.

“Tukibambwa je?” Aliuliza Suma huku akifungua mikono yake kumruhusu Sosi amkumbatie na kumvuta karibu. Alimwangalia Sosi machoni kwa macho yaliyolegea ambayo yalikuwa yanaita “njoo”!

“Hakuna mtu huku” Sosi alijibu huku akimwangushia Suma busu la taratibu, lenye unyevu kwenye midomo ya binti huyo iliyopauka. Suma alijiui kwa taratibu na upole wote huku akiguna kwa msisimko uliompitia kama umeme kuanzia utosini hadi kwenye nyayo. Alijikuta miguu yake imenyong’onyea. Moyo ulizidi kumdunda. Alijihisi kutekenywa sehemu ambazo ni bora zisitajwe hadharani. Akafungua mdom o wake zaidi na ndimi zao zikakutana, zikagongana na kuanza kuvingirishana utadhani ziko kwenye mashindano ya mabusu. Walipeana denda huku mikono yao ikipapasana mgongoni, kichwani, na karibu kila kiungo kingine cha mwili. Sospeter alijikuta “anazidiwa” kwani mzee aliyekuwa amelala aliamka utadhani kifaru mwenye hasira. Suma aliweza kuhisi kutuna kwa suruali ya Sosi, kitu ambacho kilimpagawisha.

Comments

Popular posts from this blog

Vifahamu Vitu Vidogo Vidogo Ambavyo Huzidisha Utamu wa Mahusiano Katika Mapenzi

UTAMU WA MCHEZO SEHEMU YA 2

Jinsi ya kumtoa msichana Bikra bila maumivu, wengi hawajui hili, Cheki hapa.