MAMA VANESSA SEHEMU YA 12.
“Habari zenu” Mama Vanessa alitoa salamu ya jumla.
“Nzuri” Kimaro na kimwana aliyekuja naye walijibu kwa pamoja.Kimya kikatawala kidogo kabla ya Lucas kuvunja ukimya.
“Mama Vanessa huyu anaitwa Kimaro ni rafiki wangu wa kufa na kuzikana. Mr Kimaro huyu ndio mama Vanessa mwanamke aliyeamua kuniokota mara baada ya Mishel kunitupa.
“Nashukuru sana bwana Lucas nashukuru pia kumfahamu mama Vannesa..Kimaro aliongea huku akimpa mkono mama Vanessa. Alifanya utani wake kidogo kwa kuubinya mkono kwa nguvu jambo lilofanya mama Vanesa ahisi maumivu.
“Aiseee kweli unastahili hili kuitwa mrembo mikono laini kama maini” Kimaro aliongea huku akionesha kushangaa.
Wote kwa pamoja walicheka na kufanya kuchangamka. Muhudumu alikuja tena na kumleta kinywaji mama Vanesa. Safari hii alibadilisha na kuanza kunywa wine. Stori mbili tatu za kuchekesha ziliendelea na kufanya muda kuzidi kuyoyoma. Kimaro alitumia muda huo vizuri kuwafurahisha na kuwachekesha kwa sababu moja ya vitu alivyojaliwa ni kuwafurahisha watu na kuwafanya wamsikilize kwa muda mrefu.
Wakati stori zikiendelea mama Vanessa yeye alikuwa ulimwengu mwingine kabisa. Alikuwa akiwaza ni jinsi gani atarudi Musoma hili hali muda ulikuwa umeenda sana. Aliendelea kunywa kinywaji huku akili yake ikifanya kazi ya ziada juu ya uwongo gani afanye ili mme wake amuelewe. Yaani mama Vanesa alikuwa ni mwanamke wa ajabu sana huku duniani kwa sababu ingawa mme wake alikuwa akimtenda vibaya kila mara lakini hakuwahi kuwa mkaidi. Siku zote amekuwa mtiifu na amekuwa akijishusha. Haya yote aliyafanya kwa sababu alitokea kwenye familia masikini. Alijifanya kipofu kwa kwa mabaya yote ambayo alikuwa akitendewa na mumewe. Lakini alikuwa na lake moyoni kwa kuwa muda huo yeye kujifanya boya ulikuwa umekwisha. Tayari alikuwa ameshachuma mali za kutosha. Alishajenga kwao na alishakuwa na nyumba mjini. Mumewe alimwamini sana na hakujua kuwa ipo siku atabadilika.
“Mbona mama Vanesa anaonekana kama mwenye mawazo?”Kimaro aliuliza mara baada ya kuona huyo ametulia tu.
“Hamna mimi sina mawazo yoyote tupo pamoja” Mama Vanesa alisema huku akitaka kusema kuwa anataka kuondoka. Ila aliamua kujiuliza maswali na kujijibu mwenyewe.Sasa nitaondokaje na kilichokileta huku sijakipata. Hata hatujaweka mikakati ya kumkomesha baba Vanesa. Ilibidi amuandikie sms Lucas kumueleza nia yake ya kutaka kuondoka. Lucas na yeye alimuuliza swali lile kuwa sasa ataondokaje wakati bado hatujapanga mikakati. “Mimi naona utafute njia ulale kwa sababu tayari chumba kipo.Lucas alishauri na wakati huo huo Lucas pia alianza kuchati ana Kimaro kumwambia kuwa mama Vanesa anataka kuondoka. Kimaro akasisitiza kuwa hilo haiwezi kutokea kama yeye yupo.
“Inaoenkana watu mmekaa kiunyonge nyonge sasa napendekeza tuhame kwa muda kuna mahali nasikia kuna nyama choma twendeni tukale.” Kimaro aliongea huku akiinuka na kumpa mkono msichana aliyekuja naye kisha kuanza kupiga hatua na kuondoka. Lucas alitamani kucheka lakini alijikausha na yeye akafanya kumpa mkono Mama Vanesaa.
“Leo upo na vijana wenzako huna haja ya kuwa na wasiwasi. Sahau hata mawazo ya kuumizwa kimapenzi na baba Vanessa..
“Ni sawa lakini nitamwambia nipo wapi au nimelala wapi.
“Kwanini yeye anavyoondokaga na kulala nje ya ndoa huwa anakwambai ukweli kuwa amekwenda kukusaliti?
“Hapana”
“Sasa na wewe tafuta uwongo mtakatifu”
Ilibidi na wao waanze kupiga hatua na kuondoka eneo hilo. Walivuka tena na boti na kutoka nchi kavu. Lucas alikuwa ameenda na gari hivyo waliingia kwenye gari. Mama Vanesa licha ya kuwa alikuwa amechoshwa na tabia za mumewe lakni pia mumewe alikuwa hana uwezo wa kumrizisha kitandani. Huo ulikuwa ni ukweli ambao haupingiki kuwa mume wake hakuwahi kurizisha hasa siku hizi za karibuni ingawa kipindi kile wameanza uhusiano wao alikuwa akifurahia. Alichokifanya mama Vanesa ni kuzima simu na alimtumia sms mume wake kuwa simu yake inazima chaji. Hakumwambia kuwa hatorudi nyumbani wala nini. Waliondoka na kuenda hiyo sehemu ambayo Kimaro alisema. Mama Vanesaa aliamua kuamishia mawazo yake kwenye kujipa raha usiku huo. Mpaka muda huo alikuwa hajaelewa kama Lucas anampango wa kulala naye au ndo kama vile aivyomwambia. Na kama atalala mwenyewe basi kuna umuhimu gani wa kufanya hivyo.
Waliingia sehemu ambayo palikuwa pamechangamka sana. Ilikuwa ni sehemu ambayo ilionekana ni ya gharama maana muziki laini ulikuwa ukiimbwa live. Ingawa nyimbo zilizokuwa zikiimbiwa zilikuwa ni nyimbo za zamani lakini ziliwavutia. Haraka haraka waliagiza na kuendelea kunywa huku wakisubri nyama choma. Hapo hapakuwa ana longolongo ya kusubiri muda mrefu. Nyama zilikuja na wakaendelea kula.Wakaendelea kula na kunywa.Wote walizidi kuchangamka na wakajikuta wanatamani kucheza musiki. Lucas na Kimaro wakawa tayari wamepanga mambo hayo. Akaanza Kimaro kuamka na kumchukua huyo mwanamke aliyekuwa naye na kuanza kucheza naye. Lucas na yeye akajifanya kuwa uzalendo umemshindwa.Alimnyanya mama Vanessa na kuanza kucheza naye musiki.
Walianza kucheza huku Kimaro alikuwa akirekodi lile tukio na kuchukua picha. Lengo ilikuwa ni kulipiza kisasi kwa kumrusha roho boss. Lucas alijifanya amelewa maana alikuwa akicheza na mama Vanesa kama mtu na mpenzi wake.Burudani iliendelea mpaka mida ya usiku. Kwa kuwa Kimaro siku hiyo hakutaka kukaa sana waliamua kuondoka . Waliingia kwenye gari na kitu cha kwanza walichofanya ni kuwapeleka Lucas na Mama Vanesaa kwenye ile hotel ambayo walikuwa wao mwanzo. Tayari kamera ziliwekwa kwa ajili ya kuwarekodi. Kamera ziliwekwa kisiri mradi tu kupata picha za matukio ambayo kama boss wake akiziona basi lazima atakufa kwa presha. Lucas safari hii alibadilika alikuwa tofauti kabisa na mwanzo hakuwa mtu wa kujadiliana zaidi aliongoza mpaka pale kwenye chumba walichokodi. Vitu vya mama Vanesa vilikuwa humo na hivyo kwake yeye ilikuwa ni faida lazima mwanamke huyo angeingia humo.
Waliingia wote na Lucas alifunga mlango kisha akajitupa kitandani. Alijifanya kuwa alikuwa akisikia vibaya na pombe zilikuwa zimemzidi hivyo alihitaji kupumzika. Mama Vanesa alisimama kama mlingoti kisha akatupa swali la kizushi.
“Kwa hiyo Lucas unataka kulala na mke wa boss wako chumba kimoja”
“Najua ni ngumu sana lakini naomba mama Vanesaa unikumbuke katika ufalme wako..Kama ikukupendeza unizawadie zawadi ya faraja usiku huu la ikikuchukiza basi nitalala hata chini kama sio chooni”
Maneno ya Lucas yalimtoka kwa hisia sana na alijaribu kujishusha na kuonesha kuwa alikuwa akitamani penzi la mke wa boss ingawa ni kwa hiyari sio lazima. Maneno yale yalimuuma sana mama Vanesa na akaijikuta akimuonea huruma. Alikumbuka pia jinsi kijana huyo alivyokuwa akitia huruma alipokuwa akimwelezea ni kiasi gani anapata uchungu kwa kupokonywa mke wake.Roho ya huruma ilimjia na kumfanya amsogelee pale na kuanza kumpapasapapsa. ******ITAENDELEA
“Nzuri” Kimaro na kimwana aliyekuja naye walijibu kwa pamoja.Kimya kikatawala kidogo kabla ya Lucas kuvunja ukimya.
“Mama Vanessa huyu anaitwa Kimaro ni rafiki wangu wa kufa na kuzikana. Mr Kimaro huyu ndio mama Vanessa mwanamke aliyeamua kuniokota mara baada ya Mishel kunitupa.
“Nashukuru sana bwana Lucas nashukuru pia kumfahamu mama Vannesa..Kimaro aliongea huku akimpa mkono mama Vanessa. Alifanya utani wake kidogo kwa kuubinya mkono kwa nguvu jambo lilofanya mama Vanesa ahisi maumivu.
“Aiseee kweli unastahili hili kuitwa mrembo mikono laini kama maini” Kimaro aliongea huku akionesha kushangaa.
Wote kwa pamoja walicheka na kufanya kuchangamka. Muhudumu alikuja tena na kumleta kinywaji mama Vanesa. Safari hii alibadilisha na kuanza kunywa wine. Stori mbili tatu za kuchekesha ziliendelea na kufanya muda kuzidi kuyoyoma. Kimaro alitumia muda huo vizuri kuwafurahisha na kuwachekesha kwa sababu moja ya vitu alivyojaliwa ni kuwafurahisha watu na kuwafanya wamsikilize kwa muda mrefu.
Wakati stori zikiendelea mama Vanessa yeye alikuwa ulimwengu mwingine kabisa. Alikuwa akiwaza ni jinsi gani atarudi Musoma hili hali muda ulikuwa umeenda sana. Aliendelea kunywa kinywaji huku akili yake ikifanya kazi ya ziada juu ya uwongo gani afanye ili mme wake amuelewe. Yaani mama Vanesa alikuwa ni mwanamke wa ajabu sana huku duniani kwa sababu ingawa mme wake alikuwa akimtenda vibaya kila mara lakini hakuwahi kuwa mkaidi. Siku zote amekuwa mtiifu na amekuwa akijishusha. Haya yote aliyafanya kwa sababu alitokea kwenye familia masikini. Alijifanya kipofu kwa kwa mabaya yote ambayo alikuwa akitendewa na mumewe. Lakini alikuwa na lake moyoni kwa kuwa muda huo yeye kujifanya boya ulikuwa umekwisha. Tayari alikuwa ameshachuma mali za kutosha. Alishajenga kwao na alishakuwa na nyumba mjini. Mumewe alimwamini sana na hakujua kuwa ipo siku atabadilika.
“Mbona mama Vanesa anaonekana kama mwenye mawazo?”Kimaro aliuliza mara baada ya kuona huyo ametulia tu.
“Hamna mimi sina mawazo yoyote tupo pamoja” Mama Vanesa alisema huku akitaka kusema kuwa anataka kuondoka. Ila aliamua kujiuliza maswali na kujijibu mwenyewe.Sasa nitaondokaje na kilichokileta huku sijakipata. Hata hatujaweka mikakati ya kumkomesha baba Vanesa. Ilibidi amuandikie sms Lucas kumueleza nia yake ya kutaka kuondoka. Lucas na yeye alimuuliza swali lile kuwa sasa ataondokaje wakati bado hatujapanga mikakati. “Mimi naona utafute njia ulale kwa sababu tayari chumba kipo.Lucas alishauri na wakati huo huo Lucas pia alianza kuchati ana Kimaro kumwambia kuwa mama Vanesa anataka kuondoka. Kimaro akasisitiza kuwa hilo haiwezi kutokea kama yeye yupo.
“Inaoenkana watu mmekaa kiunyonge nyonge sasa napendekeza tuhame kwa muda kuna mahali nasikia kuna nyama choma twendeni tukale.” Kimaro aliongea huku akiinuka na kumpa mkono msichana aliyekuja naye kisha kuanza kupiga hatua na kuondoka. Lucas alitamani kucheka lakini alijikausha na yeye akafanya kumpa mkono Mama Vanesaa.
“Leo upo na vijana wenzako huna haja ya kuwa na wasiwasi. Sahau hata mawazo ya kuumizwa kimapenzi na baba Vanessa..
“Ni sawa lakini nitamwambia nipo wapi au nimelala wapi.
“Kwanini yeye anavyoondokaga na kulala nje ya ndoa huwa anakwambai ukweli kuwa amekwenda kukusaliti?
“Hapana”
“Sasa na wewe tafuta uwongo mtakatifu”
Ilibidi na wao waanze kupiga hatua na kuondoka eneo hilo. Walivuka tena na boti na kutoka nchi kavu. Lucas alikuwa ameenda na gari hivyo waliingia kwenye gari. Mama Vanesa licha ya kuwa alikuwa amechoshwa na tabia za mumewe lakni pia mumewe alikuwa hana uwezo wa kumrizisha kitandani. Huo ulikuwa ni ukweli ambao haupingiki kuwa mume wake hakuwahi kurizisha hasa siku hizi za karibuni ingawa kipindi kile wameanza uhusiano wao alikuwa akifurahia. Alichokifanya mama Vanesa ni kuzima simu na alimtumia sms mume wake kuwa simu yake inazima chaji. Hakumwambia kuwa hatorudi nyumbani wala nini. Waliondoka na kuenda hiyo sehemu ambayo Kimaro alisema. Mama Vanesaa aliamua kuamishia mawazo yake kwenye kujipa raha usiku huo. Mpaka muda huo alikuwa hajaelewa kama Lucas anampango wa kulala naye au ndo kama vile aivyomwambia. Na kama atalala mwenyewe basi kuna umuhimu gani wa kufanya hivyo.
Waliingia sehemu ambayo palikuwa pamechangamka sana. Ilikuwa ni sehemu ambayo ilionekana ni ya gharama maana muziki laini ulikuwa ukiimbwa live. Ingawa nyimbo zilizokuwa zikiimbiwa zilikuwa ni nyimbo za zamani lakini ziliwavutia. Haraka haraka waliagiza na kuendelea kunywa huku wakisubri nyama choma. Hapo hapakuwa ana longolongo ya kusubiri muda mrefu. Nyama zilikuja na wakaendelea kula.Wakaendelea kula na kunywa.Wote walizidi kuchangamka na wakajikuta wanatamani kucheza musiki. Lucas na Kimaro wakawa tayari wamepanga mambo hayo. Akaanza Kimaro kuamka na kumchukua huyo mwanamke aliyekuwa naye na kuanza kucheza naye. Lucas na yeye akajifanya kuwa uzalendo umemshindwa.Alimnyanya mama Vanessa na kuanza kucheza naye musiki.
Walianza kucheza huku Kimaro alikuwa akirekodi lile tukio na kuchukua picha. Lengo ilikuwa ni kulipiza kisasi kwa kumrusha roho boss. Lucas alijifanya amelewa maana alikuwa akicheza na mama Vanesa kama mtu na mpenzi wake.Burudani iliendelea mpaka mida ya usiku. Kwa kuwa Kimaro siku hiyo hakutaka kukaa sana waliamua kuondoka . Waliingia kwenye gari na kitu cha kwanza walichofanya ni kuwapeleka Lucas na Mama Vanesaa kwenye ile hotel ambayo walikuwa wao mwanzo. Tayari kamera ziliwekwa kwa ajili ya kuwarekodi. Kamera ziliwekwa kisiri mradi tu kupata picha za matukio ambayo kama boss wake akiziona basi lazima atakufa kwa presha. Lucas safari hii alibadilika alikuwa tofauti kabisa na mwanzo hakuwa mtu wa kujadiliana zaidi aliongoza mpaka pale kwenye chumba walichokodi. Vitu vya mama Vanesa vilikuwa humo na hivyo kwake yeye ilikuwa ni faida lazima mwanamke huyo angeingia humo.
Waliingia wote na Lucas alifunga mlango kisha akajitupa kitandani. Alijifanya kuwa alikuwa akisikia vibaya na pombe zilikuwa zimemzidi hivyo alihitaji kupumzika. Mama Vanesa alisimama kama mlingoti kisha akatupa swali la kizushi.
“Kwa hiyo Lucas unataka kulala na mke wa boss wako chumba kimoja”
“Najua ni ngumu sana lakini naomba mama Vanesaa unikumbuke katika ufalme wako..Kama ikukupendeza unizawadie zawadi ya faraja usiku huu la ikikuchukiza basi nitalala hata chini kama sio chooni”
Maneno ya Lucas yalimtoka kwa hisia sana na alijaribu kujishusha na kuonesha kuwa alikuwa akitamani penzi la mke wa boss ingawa ni kwa hiyari sio lazima. Maneno yale yalimuuma sana mama Vanesa na akaijikuta akimuonea huruma. Alikumbuka pia jinsi kijana huyo alivyokuwa akitia huruma alipokuwa akimwelezea ni kiasi gani anapata uchungu kwa kupokonywa mke wake.Roho ya huruma ilimjia na kumfanya amsogelee pale na kuanza kumpapasapapsa. ******ITAENDELEA
Comments
Post a Comment